Unapoboresha Tor relay yako, na kuisogeza kwenye kompyuta tofauti, sehemu muhimu ni kuendeleza unguo za utambulisho sawa (zilizohiadhiwa kwenye "keys/ed25519_master_id_secret_key" and "keys/secret_id_key" kwenye DataDirectory yako). Kuwa na nakala za funguo za utambulisho ili uweze kurejesha relay kwa baadaye ni njia iliyopendekezwa kuhakikisha sifa za relay hazipotei.

Hii inamaanisha kwamba kama umesakisha Tor relay yako na umeweka torrc sawa na DataDirectory sawa, ndipo usakishaji utafanya kazi na relay yako itaendelea kutumia funguo ileile. Kama unataka kuchagua DataDirectory mpya, hakikisha una nakala ya funguo za zamani/ed25519_master_id_secret_key and keys/secret_id_key over.

Kama wewe ni mwendeshaji bridge, hakikisha unanakili pt_state/. Inahusisha taarifa zinazohitajika kwa ajili ya bridge yako iendelee kufanya kazi na mstari wa bridge uleule.

Zingatia: Kama ilivyo kwa Tor 0.2.7 tunatumia vitambulisho vya vipya vya relay vilivyojikita kwenye ed25519 kriptographia ya mviringo. Hatimaye watabadilisha vitambulisho vya zamani vya RSA, lakini hii hutokea kwa muda, kuhakikisha utangamano na matoleo ya zamani. Mpaka , kila relay itakapokuwa na utambulisho wote wa ed25519 (faili la funguo ya utambulisho: keys/ed25519_master_id_secret_key) na utambulisho wa RSA (faili la funguo ya utambulisho: keys/secret_id_key). Unahitaji kuwa na nakala ya vyote ili kurejesha relay yako, kubadilisha DataDirectory yako au kuhamisha relay kwenye kompyuta mpya.